You are currently viewing ABBY CHAMS AAHIDI KUFANYA MAKUBWA SONY MUSIC

ABBY CHAMS AAHIDI KUFANYA MAKUBWA SONY MUSIC

Mrembo mwenye kipaji kikubwa, Abby Chams ambaye amesaini mkataba na kampuni ya Sony Music Entertainment, amesema anajivunia kujiunga na lebo hiyo kubwa ya muziki kwani ndoto zake zinakwenda kutimia haraka.

Akizungumza mara baada ya kusaini dili hilo Juni 8, 2022, Abigial amesema anajiona mwenye bahati na anaahidi kufanya makubwa kwani kazi yake inakwenda kuwa nyepesi chini ya Sony.

“Najiona mwenye bahati ya kipekee kuwa mmoja wanafamilia wa lebo kubwa Afrika, ndoto zangu zimetimia, Ninaahidi kuwapa mashabiki wangu vitu vizuri zaidi,” alisema.

Kwa upande wake mkuu wa Sony Music Afrika Mashariki, Christine ‘Seven’ Mosha, amesema anafahamu uwezo wa binti huyo mwenye sauti nzuri ya kuvutia mashabiki hivyo anafurahi kuwa naye.

Mrembo huyo anatarajia kuachia wimbo wake mpya wa U and I Ijumaa hii, Juni 17.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke