You are currently viewing AKOTHEE KUANZA ZIARA YAKE YA KIMUZIKI JULAI MWAKA 2022

AKOTHEE KUANZA ZIARA YAKE YA KIMUZIKI JULAI MWAKA 2022

Staa wa muziki nchini Akothee ametangaza kuanza kwa ziara yake ya kimuziki mwezi Julai mwaka wa 2022 Barani Ulaya na Marekani

Akothee ameipa ziara hiyo jina la Akothee World Tour ambayo itaanza Julai 2, mwaka wa 2022 huko Munich nchini Ujerumani.

Ziara hiyo inatarajiwa kupita kwenye miji mbalimbali ikiwemo Stuttgart, Ujerumani tarehe 30 Julai, na Jonkoping, Sweden Julai 30 mwaka wa 2022.

Tour hiyo pia inatarajiwa kuzunguka kwenye miji mbalimbali nchini Marekani,Dubai, Nigeria, Tanzania, Uganda, Kenya, na Afrika Kusini ila Akothee ameahidi kuweka wazi tarehe rasmi ambayo ataanza ziara yake hiyo kwenye nchi hizo.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke