You are currently viewing AKOTHEE MBIONI KUZINDUA KITABU CHAKE

AKOTHEE MBIONI KUZINDUA KITABU CHAKE

Mwanamuziki na mfanyibiashara maarufu nchini, Akothee anatarajiwa kuzindua kitabu chake  ambacho amekipa jina la “Akothee Quotes”.

Akothee Ametumia Ukurasa Wake Wa Instagram Kuthibitisha Hilo ambapo amesema kwamba kitabu hicho kinaelezea namna ya kufanikiwa kwenye maisha katika nyanja mbalimbali.

Kwenye kitabu hicho ambacho kitazinduliwa rasmi  Juni 4, mwaka huu katika hoteli ya Eka Hotel, Akothee amesimulia kuhusu maisha yake kama mtu maarufu na maisha yake binafsi.

Hata hivyo ametoa wito kwa mashabiki kukaa mkao kula kununua kitabu cha Akothee Quotes huku akisema sehemu ambayo anaipenda kwenye kitabu hicho  ni ile ambayo inazungumzia maisha ya malezi ya watoto.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke