You are currently viewing Album ya Fik Fameica, “King Kong” yakamata namba moja Apple Music

Album ya Fik Fameica, “King Kong” yakamata namba moja Apple Music

Rapa kutoka nchini Uganda Fik Fameica ameendelea kutikisa katika vichwa vya habari kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii kwa album yake ya King Kong.

Kwa mujibu wa takwimu album ya rapa huyo King Kong imevunja rekodi na kuwa ya kwanza katika mtandao wa kusikiliza muziki  wa “Apple” kwa upande wa afrika ikiipiku album ya Burna Boy, Love Denim.

Fik Fameica ametumia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa instagram kuwashukuru mashabiki zake kwa upendo ambao wanazidi kumuonyesha kupitia album yake mpya huku akiahidi kuendelea kuwapa burudani zaidi.

Album ya King Kong iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu na mashabiki wa Fik Fameica imeingia sokoni rasmi  Oktoba 29, mwaka wa 2022 ikiwa na jumla ya mikwaju 18.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke