Verse ya Nicki Minaj kwenye ngoma ya Kanye West “Monster” ya mwaka 2010 ilikuwa ya moto sana ingawa YE hajawahi kufurahishwa na mauaji ya mrembo huyo kwenye ngoma hiyo.
Sasa Amber Rose ambaye ndiye alimleta Nicki Minaj studio kuifanya verse hiyo, amerudi tena na kufunguka mengi kuhusu sakata hilo.
Kwenye mahojiano yake na Podcast ya (Higher Learning) Amber amesema Kanye West aliwahi kumtamkia wazi kuwa, kwanini umeniletea mtu ambaye amekuja kuniua kwenye ngoma yangu?
YE: “How the f*ck did you bring in a b*tch that killed me on my own song?” Amesema.
Utakumbuka mwanamitindo na mwigizaji kutoka Marekani Amber Rose aliwahi kukaririwa mwaka 2018 akisema YE alibaki kidogo aifute verse hiyo.