You are currently viewing Annastacia Mukabwa afunga ndoa  na mpenzi wake wa siku nyingi Maurice William Juma

Annastacia Mukabwa afunga ndoa  na mpenzi wake wa siku nyingi Maurice William Juma

Mwimbaji wa nyimbo za Injili Annastacia Mukabwa, amefunga ndoa  na mpenzi wake wa siku nyingi Maurice William Juma .

Taarifa hizo zimethibitisha na marafiki zake wa karibu baada ya kuachia picha za baadhi ya matukio ya Harusi yao ambayo ilifanyika katika Kanisa Kuu la Praise huko Imara Daima, Nairobi Desemba 10.

Harusi hiyo ilihudhuriwa na waimbaji kadhaa mashuhuri wa nyimbo za Injili, akiwemo Evelyne Wanjiru, Lady Bee na Solomon Mkubwa.

Hata hivyo mastaa mbali mbali na mashabiki wake wamempongeza kwa hatua hiyo huku wakimtakia mema  na mume wake  katika safari yao ya ndoa.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke