Mwanamuziki nyota nchini Arrow Boy ameachia rasmi Cover ya album yake mpya iinayokwenda kwa jina la “Focus”
Kupitia ukurasa wake instagram Arrow Boy ametuonyesha cover ya album yake mpya huku akiwataka mashabiki zake wakae mkao wa kula kuipokea Album hiyo ambayo itaingia sokoni machi 12 mwaka wa 2022.
Licha ya kuweka wazi jina na cover ya album yake mpya, Arrow Boy hajatuambia idadi ya ngoma na wasanii aliowashirikisha kwenye album yake ya Focus.
Focus album inaenda kuwa album ya pili kwa mtu mzima Arrow Boy baada ya Hatua iliyotoka mwaka wa 2019.