You are currently viewing Ashanti akiri kuwahi kuombwa rushwa ya ngono na Mtayarishaji wa Muziki

Ashanti akiri kuwahi kuombwa rushwa ya ngono na Mtayarishaji wa Muziki

Mwanamuziki kutoka Marekani Ashanti ametoboa siri ambayo wengi walikuwa hawaifahamu, amekiri kuwahi kupitia changamoto kwenye muziki wake ikiwemo ya kuombwa rushwa ya ngono na Mtayarishaji wa Muziki ili tu apate nafasi ya kurekodi wimbo.

Kwenye mahojiano na The Breakfast Club, Ashanti amekaririwa akisema, baada ya kurekodi nyimbo mbili na Mtayarishaji huyo, ilifika wakati wa kutaka kuziweka kwenye Album na hapo ndipo Jamaa alimwambia anamtaka kimapenzi na kama akikataa ombi hilo, basi atalipia ($40k) zaidi ya KSh. Milioni 4.9 kwa kila wimbo.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke