Mkali wa muziki kutoka nchini uganda Azawi ameachia rasmi album yake mpya inayokwenda kwa jina la African music.
African Music album imebeba jumla ya mikwaju 16 ya moto huku ikiwa na kolabo nne.
Azawi amewashirikisha wasani kutoka uganda ambao ni Eddy kenzo, A Pass, Fik Fameica na bosi wa lebo ya muziki ya swangz avenue Benon Mugumbya.
Album ya “African Music” ni album ya kwanza kutoka kwa Azawi baada ya kutubariki na EP yake iitwayo Lo-Fit iliyotoka mwaka wa 2020.
Hata hivyo Album hiyo inapatikana ‘Exclusive’ kupitia mitandao yote ya kukisikiliza na kuuza muziki duniani kama vile Apple music, Boomplay, na Spotify