You are currently viewing AZIZ AZION MBIONI KUJA NA ONE DECADE CONCERT

AZIZ AZION MBIONI KUJA NA ONE DECADE CONCERT

Mwanamuziki kutoka nchini Uganda Aziz Azion, ametangaza kwamba  ana mpango wa kuja na tamasha la muziki la One Decade Concert kuadhimisha miaka 10 ya uwepo wake kwenye muziki baada ya katazo la kufanya matamasha ya muziki litakapoondolewa nchini uganda.

Mwimbaji huyo mwenye umri wa miaka 37 amedokeza kuwa kiingilio cha tamasha hilo litakuwa shillingi laki tano za kenya katika sehemu ambayo ataweka wazi hivi karibuni baada kukamilisha taratibu za kuandaa tamasha hilo.

Hitmaker huyo wa My Oxygen amesema alipaswa kufanya tamasha hilo mwaka wa 2019 lakini kwa sababu ya maswala kadhaa ambayo yalikuywa nje ya uwezo wake, alilazimika kuahirisha hadi  mwaka wa 2020.

Mwaka wa 2020 bado, tamasha hilo lilifeli kufanyika kufuatia kuzuka kwa janga la Corona ambayo ililemaza shughuli zote za kibiashara ulimwenguni kote.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke