You are currently viewing BAHATI AZUA GUMZO MTANDAONI KWA KUFUTA KILA KITU INSTAGRAM

BAHATI AZUA GUMZO MTANDAONI KWA KUFUTA KILA KITU INSTAGRAM

Staa wa muziki nchini Bahati amefuta picha na video zake kwenye mtandao wa Instagram, hatua iliyohisiwa ni ujio wake mpya.

Hatua hii ya Bahati imevuta hisia za baadhi ya mashabiki ikihisiwa kuwa huenda akaachia kazi mpya hivi karibuni baada ya kukaa kimya tangu apoteze kiti cha ubunge mathare kwenye uchaguzi mkuu uliokamilika nchini kenya.

Uamuzi wa Bahati hakujali hata picha alizopiga na mke wake, Diana B huku upande mwingine ikihisiwa kuwa pengine kuna kingine kisichohusiana na ujio wa kazi kutoka kwake.

Utakumbuka juzi kati Bahati alifunguka kuwa familia yake ipo njia panda ambapo aliwataka mashabiki kumweka kwenye maombi pamoja na mke wake Diana ambaye alikuwa mbioni kujifungua.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke