You are currently viewing BARNABA & ZUCHU WAMJIBU ERICO OMONDI ALIYEDAI BONGOFLEVA IMEULIWA NA AMAPIANO

BARNABA & ZUCHU WAMJIBU ERICO OMONDI ALIYEDAI BONGOFLEVA IMEULIWA NA AMAPIANO

Baada ya msanii wa Comedy nchini Eric Omondi kudai kuwa Amapiano imeuwa muziki wa Bongo Fleva,wasanii wa Tanzania Zuchu na Barnaba Classic wameibuka na kupinga hilo.

Wasanii hao wamesema kwamba wanachokifanya kwa sasa ni kutaka kukimbizana na nyakati zilizopo kwani kuwa kwenye kiwanda cha muziki ambacho kina ushindani kunahitaji msaani kuwa na ubunifu

Barnaba kupitia ukurasa wake wa Instagram ameandika “Bongo Fleva bado ina nguvu sana kuliko Amapiano. Watu wajue Amapiano sio aina ya muziki bali kwa lugha rahisi ni mixing za Dj’s wa Arika Kusini so haitoweza kuuwa Bongo Fleva”

Kwa upande wa Zuchu ameandika kuwa “Bongo Fleva haitotokea kufa wasanii wanabadilika hii inaitwa mabadiliko, kujaribu ladha mpya hakujawahi kuuwa soko la muziki. Acha wasanii wajaribu vitu vipya ndio mabadiliko hayo”

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke