You are currently viewing BEB COOL MBIONI KUWAFUNGULIA MASHTAKA WANAOMPAKA TOPE NCHINI UGANDA

BEB COOL MBIONI KUWAFUNGULIA MASHTAKA WANAOMPAKA TOPE NCHINI UGANDA

Mwanamuziki Moses Ssali maarufu Bebe Cool ni mmoja wa wasanii waliokosolewa zaidi nchini Uganda, lakini huenda wanaomchafulia jina wakijipata hatiani hivi karibuni.

Katika mahojiano ya hivi  karibuni na MwanaYouTube wa eneo hilo, bosi huyo wa Gagamel ameeleza kuwa ameanza kukusanya ushahidi dhidi ya wanahabari ambao wamekuwa wakimpaka tope kwa tuhuma za uongo.

“Nimejenga brand yangu kwa muda mrefu sana na kwa mwandishi yeyote wa habari kuja kuniongelea upuuzi, nawaahidi nitawapa funzo. Ninakusanya ushahidi, na watalipa,” alisema.

Hata hivyo Bebe Cool amesema washukiwa wakuu ni watangazaji wa redio na TV ambao wamekuwa wakitoa maoni hasi dhidi yake.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke