You are currently viewing Ben Pol akanusha kukamilika kwa talaka yake na Arnelisa Muiga

Ben Pol akanusha kukamilika kwa talaka yake na Arnelisa Muiga

Mwimbaji wa Bongofleva, Ben Pol amejitokeza na kusema kuwa hajapata taarifa yoyote kuhusu kukamilika kwa talaka na aliyekuwa mke wake, Anerlisa.

Wiki iliyopita Anerlisa ambaye ni binti wa seneta wa Nakuru Tabitha Karanja alitangaza kuwa mchakato wa talaka yake na Ben Pol umekamilika.

“Mimi pia naona ripoti hizi mtandaoni. Sijafahamishwa rasmi au kwa njia isiyo rasmi. Sijui hayo mawasiliano aliyapata wapi maana hata mahakama niliyofungua kesi ya talaka haifahamu taarifa hizo,” Ben Pol aliambia Nation.

Utakumbuka wawili hao walifunga ndoa Mei 2020 katika Kanisa Katoliki la St Gaspar huko Mbezi Beach, Tanzania.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke