You are currently viewing BIEN AWAPA SOMO VIJANA WALIO CHINI YA UMRI WA MIAKA 30

BIEN AWAPA SOMO VIJANA WALIO CHINI YA UMRI WA MIAKA 30

Mwimbaji mkuu wa Kundi la Sauti Sol nchini Kenya Bien amesema hashauri watu waliopo katika umri wa miaka ya ishirini kuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi kwani ni kupotezeana muda.

Bien amesema watu walio katika umri huo wanapaswa kujijali wenyewe na kusafiri kwa kuwa mtu aliyeko katika umri huo bado anajitafuta ajue kitu gani hasa anakihitaji. “Siwezi kumpa ushauri mtu mwenye umri wa miaka ishirini awe kwenye mahusiano, ni kupoteza muda, angalau fanya kazi, usafiri pia uwe na watu wengine huku na huko.” alisema Bien.

Aidha aliongeza kwamba mtu akiwa katika umri huo hajitambui na mtu aliye naye pia hajitambui “Unadhani unafanya nini? Mnajaribu kusuluhisha mambo pamoja lakini mwisho wa siku yaani nadhani ni bora kuwa peke yako ikiwa uko katika miaka ya 20” alimaliza Mwanamuziki huyo.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke