You are currently viewing BIEN WA SAUTI SOL AWATAKA WASANII WA KENYA KUIMBA NYIMBO ZA KIINGEREZA

BIEN WA SAUTI SOL AWATAKA WASANII WA KENYA KUIMBA NYIMBO ZA KIINGEREZA

Mwanamuziki wa Sauti Sol, Bien ametoa changamoto kwa wasanii nchini kuanza kutumia lugha ya kiingereza kwenye nyimbo zao ili muziki wa Kenya uweze kufika mbali zaidi.

Bien amesema licha ya wasanii wa Kenya kutoa muziki mzuri wengi wao wamekuwa wakitumia lugha ya Sheng kwenye nyimbo zao jambo analosema limewafanya wasanii kushindwa kutanua wigo wa muziki wao kimataifa.

Katika hatua nyingine Bien amekiri kuwa hakuwa anajitambua kimuziki kabla ya wasanii wa kundi la Sauti Sol kuanza kufanya kazi zao kama wanamuziki wa kujitegemea.

Hitmaker wa “Inauma” amesema amejifunza mambo mengi kama msanii huru ikiwemo kutayarisha na kuandilka nyimbo zake mwenyewe.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke