You are currently viewing Catherine Kusasira akanusha kuwadharau mashabiki kwa vibunda vya pesa

Catherine Kusasira akanusha kuwadharau mashabiki kwa vibunda vya pesa

Msanii mkongwe kwenye muziki nchini Uganda Catherine Kusasira amekanusha madai ya kuwadharau watu mitandaoni baada ya kuonekana akijigamba na vibandu vya pesa.

Kwenye mahojiano yake hivi karibuni Kusasira amedai kitendo chake cha kuwaonesha mashabiki  kibunda cha pesa mtandaoni ilikuwa ni njia ya kutengeneza mazingira ya tamasha lake la muziki kuzungumziwa mtandaoni na sio vinginevyo.

Mrembo huyo amesema pesa hizo alikopeshwa na promota Baalam kwa ajili ya kufadhili tamasha lake la muziki, hivyo hakuwa na nia ya kuwavunjia heshima mashabiki.

Kauli yake imekuja mara baada ya mashabiki kumshambulia mtandaoni alipokiri kuwa nyumba yake inapigwa mnada hivi karibuni kutokana na madeni anayodaiwa na benki.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke