You are currently viewing CEO WA BONFIRE ADVENTURE AKIRI KUWA MMLIKI WA MATATU ILIYONUNULIWA NA WILLY PAUL

CEO WA BONFIRE ADVENTURE AKIRI KUWA MMLIKI WA MATATU ILIYONUNULIWA NA WILLY PAUL

Sakata la Willy Paul kudaiwa kununua matatu ambayo imetumika imechukua mkondo mpya baada ya bosi wa Bonfire Adventures Simon Kabu kukiri hadharini yeye ndio mmiliki halisi wa matatu hiyo.

Kupitia posti ya msanii Willy Paul kwenye mtandao wa Instagram Kabu ameandika ujumbe wa kumpongeza msanii huyo kwa hatua ya kuwekeza kwenye biashara ya matatu ambapo ameenda mbali zaidi na kujinadi kuwa kabla ya Willy Paul kununua matatu hiyo yeye ndio alikuwa anamiliki.

Ujumbe huo umezua hisia mseto mitandaoni ambapo baaadhi ya wakenya wameonekana kumkosoa Kabu kwa madai ya kumvunjia heshima Willy Paul huku wengine wakiendelea kumponda msanii huyo wakihoji kuwa walikuwa na fahamu kuwa matatu hiyo ishatumika.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke