You are currently viewing CHAMA CHA WANAMUZIKI UGANDA UMA YATANGAZA TAREHE YA KUFANYIKA KWA UCHAGUZI

CHAMA CHA WANAMUZIKI UGANDA UMA YATANGAZA TAREHE YA KUFANYIKA KWA UCHAGUZI

Tume ya uchaguzi katika Chama cha Wanamuziki nchini Uganda (UMA) hatimaye, imetangaza tarehe mpya ambayo uychaguzi sambamba na mdahalo wa wagombea wa urais katika chama hicho utafanyika.

Hapo awali, mdahalo huo ulipangwa kufanyika mwishoni mwa mwezi Aprili mwaka huu lakini haukufanyika kwa sababu zilizokuwa nje ya tume hiyo.

Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi katika chama cha UMA Bwana. Jeff Geoffrey Ekongot ameeleza kuwa mjadala huo utafanyika Mei 21 kabla ya zoezi la upigaji wa kura kung’oa nanga Mei 23 mwaka huu.

Uongozi wa chama cha UMA hata hivyo umeshindwa kufafanua ikiwa upigaji kura katika chama hicho utafanyika kwa njia ya kidijitali, au kwa mfumo wa kawaida wakupanga foleni kwenye vituo vya kupiga kura.

Utakumbuka wasanii King Saha na Cindy Sanyu wanatarajiwa kumenyana kwenye kinyang’anyiro cha urais katika chama cha uma ambapo mshindi katika uchaguzi huo ataongoza chama hicho kwa miaka miwili na nusu.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke