You are currently viewing CHIDI BENZ AWABARIKI MASHABIKI NA WA2 WANGU ALBUM

CHIDI BENZ AWABARIKI MASHABIKI NA WA2 WANGU ALBUM

Album mpya ya rapa Chidi Beenz iitwayo WA2 WANGU imetoka rasmi na sasa inapatikana kupitia majukwaa mbalimbali ya ku-stream muziki mtandaoni.

Album ya WA2 WANGU yenye jumla ya nyimbo 18, ina kolabo 5 pekee, Chidi akiwapa mashavu wasanii kama Baddest, Brian Simba na wengineo kusikika kwenye album hiyo.

Hata hivyo, Chidi tayari alishaachia nyimbo 6 toka kwenye album hiyo, ambazo ni Nahamia Bar, Jirani, Walete, One, King of the Jungle na Hilo Ngoma.

Rapa Chidi Beenz ambaye ni mshindi mara nne Kill Music Awards kupitia tuzo ya msanii Bora wa Hip Hop nchini Tanzania, album yake hii mpya (Wa2 Wangu) inaifuata album ya “Dsm Stand Up” ambayo ndio album yake ya kwanza kuiachia kwenye muziki wake, ilitoka mwaka 2010.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke