You are currently viewing CHRIS BROWN AMUUNGA MKONO KYRIE IRVING KUKATAA KUCHANJWA

CHRIS BROWN AMUUNGA MKONO KYRIE IRVING KUKATAA KUCHANJWA

Chris Brown amemuunga mkono mcheza Kikapu Kyrie Irving ambaye amegoma kuchanjwa chanjo ya COVID-19.

Kupitia Insta Stories yake kwenye mtandao wa Instagram Chris Brown amesema ana simama na nyota huyo wa Brooklyn Nets na kumuita shujaa wa ukweli.

Kyrie Irving anaendelea kuvigusa vichwa vya habari duniani kwa kuigomea chanjo ya COVID-19 ambayo imefanywa kuwa lazima kwa wana michezo wote, hivyo kuweka hatiani mustakabali wake wa kucheza kwenye ligi hiyo hasa michezo ya nyumbani kwa sheria za Jiji la New York.

Staa huyo ameitaja sababu ya kugoma kuchanjwa, akisema kuwa mtu hapaswi kulazimishwa kufanya jambo lolote kwenye mwili wake, na anasimama na wote ambao wanaamini kipi ni sahihi.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke