You are currently viewing CONTE ATANGAZWA KOCHA MPYA TOTTENHAM

CONTE ATANGAZWA KOCHA MPYA TOTTENHAM

Klabu ya Tottenham imemtangaza Antonio Conte kuwa kocha wake mpya akichukua nafasi ya Nuno Espirito Santo aliyefukuzwa kazi Novemba mosi mwaka huu.

Kocha huyo wa zamani wa Klabu za Juventus, Chelsea na Inter Milan amesaini kandarasi ya miezi 18.

Kocha Nuno Espirito Santo amefungashiwa virago na Klabu hiyo ya Jijini London ikiwa ni miezi minne tangu alipoanza kuinoa timu hiyo.

Kocha huyo ameiongoza Spurs katika michezo 17, ameshinda michezo 8, kafungwa 7 na kutoka sare michezo 2 huku timu hiyo ikifunga magoli 21 na kufungwa 23.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke