You are currently viewing DADDY OWEN AWASHAURI MASTAA KUACHA KUISHI MAISHA YA KUIGIZA MTANDAONI

DADDY OWEN AWASHAURI MASTAA KUACHA KUISHI MAISHA YA KUIGIZA MTANDAONI

Mwimbaji wa nyimbo za injili nchini Daddy Owen amewashauri mastaa kurudisha mkono kwa jamii kwa kutoa misaada kwa watu wenye uhitaji.

Kupitia instagram Daddy Owen amesema hatua hiyo itawapa motisha wakenya kuwasaidia wakati matatizo badala ya kuisha maisha ya kuigiza kwenye mitandao ya kijamii.

Hitmaker huyo wa Yahweh amesema kipindi alijipata kwenye matatizo hakuna staa hata mmoja alijitokeza kumsaidia ila anamshukuru mungu mashabiki zake ndio walikuwa mstari wa mbele kumshika mkono hadi akarudi katika hali yake ya kawaida.

Daddy Owen ametoa kauli hiyo akijibu swali la mchekeshaji Creative Terrence ambaye alitaka kufahamu ni kitu gani inawafanya wakenya kutowasaidii mastaa mbali mbali nchini wakati wana changamoto katika maisha.

Swali la Terrence liliibua hisia mseto miongoni mwa wakenya mtandaoni ambao wamehoji kuwa wasanii wanaishi maisha ya kifahari kwenye mitandao ya kijamii jambo limewafanya wengi wake kutoamini kama kweli huwa wanapata maishani.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke