Mwimbaji wa nyimbo za injili kutoka Kenya David Wonder ameachia rasmi Album yake mpya iitwayo “Mwanzo”
Album hiyo ina jumla ya nyimbo 12 ambapo ni wanamuziki 4 pekee ndio waliopata shavu la kushirikishwa ndani ya album hiyo ambao ni Guardian Angel, Jabidii, Moji ShortBabaa na Hakuna Matata.
Miongoni mwa watayarishaji waliohusu kuipika Album hiyo ni pamoja na Shallz baro, Sean on the Beat na Alexis on the Beat.
Mwanzo ambayo ni Album ya kwanza katika safari ya muziki ya David Wonder tayari inapatikana kupitia digital platforms zote za kupakua na kusikiliza muziki duniani.