You are currently viewing DAVIDO ATANGAZA KUGAWA PESA ZOTE ALIZOPOKEA TOKA KWA MARAFIKI NA MASHABIKI

DAVIDO ATANGAZA KUGAWA PESA ZOTE ALIZOPOKEA TOKA KWA MARAFIKI NA MASHABIKI

Kwa kawaida, kwenye kila sherehe au matatizo, suala la michango huwa ni kigugumizi kikubwa kwa watu wengi Duniani

Hii imekua tofauti kidogo kwa staa wa muziki kutoka nchini Nigeria Davido Ambaye amekuja na mbinu tofauti ya kupata zawadi kutoka kwa marafiki zake kwenye siku ya Kumbukumbu ya kuzaliwa kwake.

Goodnews ni kwamba Davido tayari amepokea kiasi cha (Naira 181M) zaidi ya shillingi millioni 49 kutoka kwa marafiki zake wa karibu pia mashabiki wa muziki ikiwa ni siku mbili tangu atangaze kuomba achangiwe pesa kwa ajili ya kusheherekea siku yake ya kuzaliwa, Novemba 21 mwaka huu.

Sasa huenda Davido asizitumie kabisa pesa hizo kama ambavyo alikuwa amepanga, kupitia ukurasa wake wa Twitter  ametangaza kuwa anaweza kuzigawa kwa wenye uhitaji.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke