You are currently viewing DIAMOND MBIONI KUFANYA KOLABO NA RIHANNA

DIAMOND MBIONI KUFANYA KOLABO NA RIHANNA

Mwanamuziki wa Bongofleva Diamond Platnumz ametangaza kushirikiana na Rihanna kwenye Album yake ijayo.

Akizungumza na BBC akiwa huko nchini Uingereza Diamond Platnumz amesema kuwa tayari ameshaweka mambo sawa kukamilisha kolabo na staa huyo mkubwa wa muziki duniani na anaamini itakuwa ni moja kati ya nyimbo kubwa kuwahi kutokea.

“Napenda kufanya kazi na Rihanna, naona itakuwa nyimbo kali sana. Natumaini kama sio kwenye album yangu hii ijayo au nyingine tunaweza kushirikiana. Tumeshafanya mazungumzo toka mwaka jana kama sikosei. Anaweza kukosekana kwenye album hii kwasababu ya hali aliyonayo lakini kwa album inayofuata naamini tutakuwa pamoja”, amesema Diamond

Diamond kwa sasa yupo nchini Uingereza kwa ajili ya kui-promote EP yake mpya FOA ambayo ameiachia wiki chache zilizopita.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke