You are currently viewing Diana Bahati aongoza kwa idadi ya subscribers Youtube upande wa wasanii wa kike nchini

Diana Bahati aongoza kwa idadi ya subscribers Youtube upande wa wasanii wa kike nchini

Mwanamitandao aliyegeukia muziki Diana Bahati ametokea kwenye orodha ya wasanii wa kike walio na subscribers wengi barani Afrika.

Kwa mujibu wa The Top Chart, Diana B anashikilia nafasi ya 8 akiwa na jumla ya subscribers elfu 783 nyuma ya Zuchu, Yemi Alade, Sinach, Tiwa Savage, Simi na Nandy ambao wanaongoza kwa idadi ya subscribers kwa wasanii wa kike barani Afrika.

Kwa matokeo hayo Diana B ndiye msanii anayeongoza nchini kwa idadi ya subscribers kwenye mtandao wa Youtube kwa upande wasanii wa wakike.

Diana B ambaye alijiunga na mtandao wa youtube Agosti 19 mwaka 2019, mpaka sasa ana jumla ya watazamaji millioni 119, 452, 136 kupitia kazi zake ambazo anazipakia kwenye mtandao huo.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke