You are currently viewing DOGO RICHIE ATOA CHANGAMOTO KWA WASANII WA KENYA KUWA WABUNIFU WA KUTENGENEZA MATUKIO

DOGO RICHIE ATOA CHANGAMOTO KWA WASANII WA KENYA KUWA WABUNIFU WA KUTENGENEZA MATUKIO

Mwanamuziki kutoka Kenya Dogo Richie amesema wasanii nchini humo wanawapa Bloggers wakati mgumu kwa kukosa  ubunifu na kupanga matukio yatakayo wapa nafasi ya kuzungumziwa katika mitandao ya kijamii.

Kwenye mahojiano ya hivi karibuni Ndogo Richie amesema kuwa amesikitishwa na hatua ya mashabiki wengi wa mziki hapa nchini kupenda kusoma tarifaa za burudani katika mitandao ya Udaku ya nchini Tanzania.

Hitmaker huyo wa ngoma ya “Bilnaden” amesema kuwa kwa sasa ni vigumu kwa msanii kupata mafanikio makubwa pasi na kuwa na matukio yatakao mfanya awe gumzo kwa mashabiki zake.

Hata hivyo amewapa changamoto wasaani kuwa wabunifu ili kuwapa bloggers maudhui ya burudani yatakayo jenga gumzo kwa mashabiki wao

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke