Rapa Drake ndiye mfalme wa Spotify nchini Marekani kwa mwaka 2022, mtandao huo umetoa takwimu za wasanii na nyimbo zilizosikilizwa zaidi kwa mwaka huu Duniani.
Drake anaongoza kwa Marekani akifuatiwa na Taylor Swift pamoja na Bad Bunny. Kanye West na The Weeknd wanaikamilisha Top 5.
Kwa upande wa Dunia nzima, Bad Bunny anaongoza kwa kuwa na streams nyingi zaidi (18.5 Billion) kwa mwaka huu pia ikiwa ni miaka mitatu mfululizo kwenye nafasi hiyo.