Bilionea wa teknolojia Elon Musk amesemaleo kwamba moja ya kampuni zake itaweza katika miezi sita kuwa na uwezo wa kupandikiza kifaa kwenye ubongo wa mwanadamu kitakachoruhusu mawasiliano na kompyuta.
Kifaa hicho kilichotolewa na kampuni ya Neuralink ya Musk, kitaruhusu mtumiaji kuwasiliana moja kwa moja na kompyuta kupitia mawazo yao, alisema.
“Tumewasilisha nadhani karatasi zetu nyingi kwa FDA (Mamlaka ya Chakula na Dawa ya Marekani) na tunafikiri pengine katika muda wa miezi sita tunapaswa kuwa na Neuralink yetu ya kwanza katika binadamu.” alisema katika wasilisho la kampuni.
“Tumekuwa tukifanya kazi kwa bidii ili kuwa tayari kwa mwanadamu wetu wa kwanza mwenye kipandikizi hiki (implant), na ni wazi tunataka kuwa waangalifu sana na hakika kwamba itafanya kazi vizuri kabla ya kuweka kifaa ndani ya mwanadamu.” alisema Musk.