You are currently viewing England kukutana na Senegal kwenye hatua ya 16 bora Kombe la Dunia 2022

England kukutana na Senegal kwenye hatua ya 16 bora Kombe la Dunia 2022

Timu ya Taifa ya Senegal imekuwa timu ya kwanza ya Afrika kufuzu kwenye hatua ya 16 Bora Kombe la Dunia mwaka huu baada ya kupata ushindi wa 2-1 dhidi ya Ecuador katika mchezo wa mwisho wa kundi A

Matokeo hayo yameifanya Senegal kumaliza wa pili katika kundi hilo kwa kufikisha alama 6 nyuma ya Uholanzi waliomaliza wakiwa vinara na alama 7 baada ya kuwazaba wenyeji Qatar 2-0 katika mchezo mwingine wa kundi hilo.

Wakati huo huo Timu ya Taifa ya England imefanikiwa kutinga hatua ya 16 Bora michuano ya Kombe la Dunia kwa kuizaba Wales 3-0 kwenye mchezo wa mwisho wa kundi B

Mabao mawili ya Marcus Rashford na moja la Phil Foden yametosha kuipa alama zote tatu England na kumaliza vinara kwenye msimamo wa kundi hilo kwa kufikisha alama 7

Sasa England atakutana na wawakilishi wa Afrika timu ya Taifa ya Senegal kwenye hatua ya 16 bora

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke