Oktoba 30 mwaka wa 2021 Staa wa muziki nchini Exray Taniua alitubariki na singo inayokwenda kwa jina la Sipangwingwi akiwa amewashirikisha wasanii Sylvia Ssaru na Trio Mio.
Goods news ni kwamba Wimbo huo umefanikiwa kufikisha jumla ya streams millioni moja kwenye mtandao wa kupakua na kusikiliza muziki wa Boomplay Kenya.
Sanjari na hilo wimbo wa Sipangwingwi pia unazidi kufanya vizuri kwenye mtandao wa youtube kwani mpaka sasa video yake imeweza kutazamwa zaida ya mara millioni 1.9 tangu ipakiwe kwenye mtandao huo.
Huu ni muendelezo mzuri kwa Exray ambaye katika siku za hivi karibuni amekuwa akiachia nyimbo mfululizo bila kupoa.