You are currently viewing FIFA yaanza uchunguzi juu ya sakata la Salt Bae kuingia uwanjani kwenye fainali ya Kombe la Dunia

FIFA yaanza uchunguzi juu ya sakata la Salt Bae kuingia uwanjani kwenye fainali ya Kombe la Dunia

Fifa inachunguza jinsi mpishi maarufu Salt Bae na watu wengine kadhaa walipata “nafasi isiofaa” kufika uwanjani mwishoni mwa fainali ya Kombe la Dunia nchini Qatar.

Salt Bae, mpishi wa Uturuki ambaye jina lake halisi ni Nusret Gokce, alionekana katika picha akiwa ameshika na kubusu kombe la Kombe la Dunia akisherehekea na wachezaji wa Argentina baada ya ushindi wao dhidi ya Ufaransa.

Sheria za Fifa zinasema kombe hilo linaweza tu kushikiliwa na kundi la watu “walioidhinishwa”, wakiwemo washindi wa mashindano, maafisa wa Fifa na wakuu wa nchi.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke