You are currently viewing Filamu ya Wakanda kuzinduliwa Nigeria

Filamu ya Wakanda kuzinduliwa Nigeria

Filamu maarufu ya ‘Black Panther: Wakanda Forever’ inayosubiriwa kwa hamu kubwa na wapenzi wa filamu Duniani kote iliyotayarishwa na Marvel Studio’s, inatarajiwa kuzinduliwa rasmi nchini Nigeria katika jiji la Lagos, kabla ya kutolewa kwake katika sinema ifikapo Novemba 11 mwaka huu.

Kwa mujibu wa taarifa, uzinduzi huu unatajwa kuwa ni wa Dunia nzima, na hayo yamebainishwa na Kampuni ya The Walt Disney wakishirikiana na Africa International Film Festival (AFRIFF) pamoja na FilmOne Entertainment.

Waanzilishi wenza wa FilmOne Entertainment, Moses Babatope na Kene Okwuosa, walielezea shauku yao kuhusu onyesho la kwanza na kutolewa kwa filamu hiyo, wakibainisha kuwa ni hatua muhimu kwa Afrika Magharibi. “Tunafuraha na tumejitolea kikamilifu kufanya kazi na Kampuni ya The Walt Disney kutoa onyesho la kwanza la Kiafrika.”

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke