You are currently viewing FOBY AACHIA RASMI EP YAKE MPYA “ME, MYSELF AND I

FOBY AACHIA RASMI EP YAKE MPYA “ME, MYSELF AND I

Msanii wa Bongo Fleva, Frank Fredrick maarufu kama Foby,ameachia rasmi EP yake mpya inayokwenda kwa jina la Me Myself and I.

Me Myself and I EP ina jumla ya ngoma 5 ambazo amezifanya kama msanii wa kujitegemea.

Ep hiyo ina ngoma kama Joto, Muda, Put It Down,Nitamsea wapi  na inapatikana kwenye majukwaa yote ya kupakua na kusikiliza muziki mitandaoni.

Me Myself and I ambayo ni Ep ya pili kwa  mtu mzima Foby  inatoka siku chache tangu atoe ombi kwa wasanii wenzake wasitoe EP zao katika kipindi cha siku 10.

Mkali huyo wa ngoma ya “Kutamu” alitoa ombi hilo la siku 10, yaani kuanzia Desemba 2 hadi 12 mwaka huu.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke