Rapa kutoka nchini marekani French montana ametangaza kuachia album yake mpya November 12, mwaka huu
French amewajuza taarifa hiyo mashabiki zake kupitia ukurasa wake wa Instagram ambapo amesema album hiyo ameipa jina la “Thet Got Amnesia”
Kwa mujibu wa French Montana Album hiyo inaelezea changamoto ya kiafya ambayo aliipitia miaka miwili iliyopita ambayo ilimfanya kupoteza kumbukumbu na kulazwa ICU.
Hii itakuwa ni Album ya nne kwa mtu mzima French Montana baada ya Excuse My French ya mwaka wa 2013,Jungle Rules ya mwaka wa 2017 na Montana ya mwaka wa 2019