You are currently viewing GRAVITY OMUTUJJU AFUNGUKA KUHUSU AFYA YAKE YA AKILI

GRAVITY OMUTUJJU AFUNGUKA KUHUSU AFYA YAKE YA AKILI

Rapa kutoka nchini Uganda Gravity Omutujju amefunguka tusiyoyajua kuhusu maisha yake.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram omutujju ametoa ya moyoni kwa kusema kuwa amekuwa akipambana na msongo wa mawazo licha ya kuendelea na harakati zake za kuachia nyimbo kila mara.

Hitmaker huyo wa ngoma ya “Tusimbudde” ameenda mbali zaidi na kudai kwamba amekuwa akiishi kwa hofu kutokana na madeni yanayomuandamana tangu afilisike kiuchumi kipindi cha corona.

“Nina huzuni, hofu na wasiwasi, lakini nitamwambia nani?

Mchezo ni mchezo! Sanaa lazima iundwe. Tumshangilie Mungu daima kwa kujidhirisha kuwa mwenye nguvu na hodari kila wakati.” Ameandika kupitia mitandao yake ya kijamii.

Mashabiki wake na watu mashuhuri wamempongeza kwa kuweka wazi safari yake kupambana na msongo wa mawazo huku wakimtakia afueni ya haraka kutoka kwa hali anayopitia kwa sasa.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke