You are currently viewing GRAVITY OMUTUJJU AKIRI KUKATAA TAMAA KWENYE MAANDALIZI YA TAMASHA LAKE

GRAVITY OMUTUJJU AKIRI KUKATAA TAMAA KWENYE MAANDALIZI YA TAMASHA LAKE

Rapa Gravity Omutujju amefunguka na kudai kwamba nusura ajiondoe kwenye tamasha lake lijalo kutokana na changamoto za promota wake anayejulikana kama Norbert.

Katika mahojiano yake hivi karibuni Omutujju amesema Promota huyo amekuwa akihujumu tamasha lake kwa kuamini maneno ya watu kuwa amekuwa akitoa tiketi za bure kwa mashabiki, jambo lililomfanya Nobert kutofanya maandalizi mazuri ya onesho hilo.

Hitmaker huyo wa “Tusimbudde” amesema alilazimika kumrejesha promota huyo baadhi ya pesa za maandalizi ya tamasha lake ambapo amedai kwamba kwa sasa anafanya kazi na promota Balaam Barugahare ambaye aliingilia kati kumsaidia kwani angehairisha onesho lake ingeathiri chapa yake ya muziki,

Tamasha la Gravity linatarajiwa kufanyika Oktoba mosi mwaka wa 2022 huko Cricket Oval, Lugogo.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke