You are currently viewing HAMISA MOBETTO MBIONI KUACHIA EP YAKE MPYA

HAMISA MOBETTO MBIONI KUACHIA EP YAKE MPYA

Mwimbaji wa Bongofleva, Hamisa Mobetto amethibitisha kuachia Extended Playlist (EP) yake mpya wiki hii.

Hamisa amebainisha hayo akizungumza na waandishi wa habari alipokuwa akitangaza kupata dili nono la ubalozi wa Kampuni ya “House of beauty”

“Wiki ijayo natoa EP yangu, itakuwa ni ya kwanza tangia nimeanza safari yangu ya muziki, tulikuwa tunabishana kati ya kutoa albamu au tutoe EP, kwa hiyo naona jambo limekimbilia kwenye EP” amesema Hamisa.

Mbali na muziki, milango ya kibiashara inazidi kufunguka kwa mwanamitindo huyo kwani ukiachilia mbali kuwa balozi wa bidhaa za urembo pia ni balozi wa kinywaji cha kishua cha Belaire.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke