You are currently viewing Hanstone adai kuibiwa wimbo na Diamond Platnumz

Hanstone adai kuibiwa wimbo na Diamond Platnumz

Msanii wa Bongofleva Hanstone ameibuka na madai ya kwamba Diamond Platnumz ameiba wimbo wake kwenye kazi yake mpya “CHITAKI” ambayo ameidokeza kwenye mitandao ya kijamii.

Kupitia insta story yake, Hanstone ameanika wazi hilo kwa kuweka kipande cha wimbo wake uitwao “NATETEMEKA” ambapo kwenye file inaonesha aliufanya mwaka 2019.

Utakumbuka Hanstone na Diamond walikuwa na ukaribu ambapo Hanstone alikuwa anatajwa kuwa angesainishwa na lebo ya WCB lakini baada ya kutokea utofauti wa pande zote mbili dili hilo lilitajwa halikuweza kukamilika.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke