Ni takribani miaka 25 imepita tangu rappa 2Pac Shakur aage dunia, alifariki mwaka 1996, na enzi za uhai wake album yake ya mwisho kuiachia ilikua ni “All eyes on Me” ambayo ilitoka Februari mwaka wa 1996.
Licha ya kwamba hatupo nae duniani, huenda hivi karibuni ukazipata kazi MPYA za rappa huyo.
Desemba mosi mwaka huu imeingizwa sokoni Hard Drive iliyokuwa ikimilikiwa na 2Pac Shakur enzi za uhai wake, ni Hard Drive yenye uwezo wa GB 83, ikiwa ina kazi MPYA za kimuziki za rappa huyo kuanzia audio na video ambazo hakuwahi kuzitoa.
Hard Drive hiyo imeingizwa sokoni kwa gharama ya Dola Milioni 1 ambazo ni takribani milioni 112 kwa pesa ya Kenya.