You are currently viewing HARMONIZE AGEUKIA FANI YA UIGIZAJI, ATANGAZA KUJA NA FILAMU

HARMONIZE AGEUKIA FANI YA UIGIZAJI, ATANGAZA KUJA NA FILAMU

Mwanamuziki na Rais wa lebo ya Konde Music Worldwide Harmonize ametangaza kuingia kwenye fani ya uigizaji muda wowote kutoka sasa.

Harmonize ambaye kwa sasa anatamba na kibao chake Women alichoshirikiana na Otile Brown ameweka wazi hilo kupitia InstaStory yake ambapo ameandika kuwa filamu hiyo kwa mara ya kwanza itaoneshwa kupitia mtandao wa Ceek.

Harmonize ameandika “Nimechoka kusubiri filamu yangu ya kwanza. Itakuwa kali sana, tukutane Ceek hivi karibuni jisajili sasa”

Kampuni ya Ceek ni kampuni  ambayo inajihusisha na maswala ya burudani kama kurusha matukio ya mubashara mtandaoni, kuandaa matamasha, na kutengeneza headphones.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke