You are currently viewing HARMONIZE ATANGAZA UJIO WA TAMASHA LAKE MWAKANI

HARMONIZE ATANGAZA UJIO WA TAMASHA LAKE MWAKANI

Nyota wa muziki wa Bongofleva Harmonize ametangaza ujio wa tamasha lake liitwalo Afro East Carnival ambapo ameweka wazi kwamba litafanyika Februari 14 mwaka 2022.

Kwenye andiko lake kupitia insta story kwenye mtandao wa Instagram, Konde Boy amesema tamasha hilo litawajumuisha wakali wa muziki Afrika Mashariki kwenye uwanja mmoja Jijini Dar Es Salaam.

Hii si mara ya kwanza kwa Harmonize kupanga kufanyika kwa tamasha kubwa la muziki nchini, August 4 mwaka wa 2020 aliitambulisha rasmi Harmo night Carnival ambayo ilipangwa kufanyika mwishoni mwa mwaka jana kwa siku tatu mfululizo.

Hata hivyo tamasha hilo halikufanyika kwa sababu ambazo hadi leo hazijawekwa wazi.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke