Huenda mapokezi ya album ya High School kutoka kwa mwanamuziki Harmonize yalikuwa makubwa katika mtandao wa Boomplay ukilinganisha na album yake ya kwanza ya ‘Afro East’
Hili limekuja kufuatia Album hiyo kufikisha zaidi ya streams Million 10 katika mtandao wa Boomplay Tanzania ikiwa ni mwezi mmoja tangu alivyo iachia rasmi live kupitia ukurasa wake wa Instagram akiwa nchini marekani.
Album yake ya kwanza Afro East’ ina streams zaidi ya million 2.6 tangu iachiwe rasmi machi 14 mwaka wa 2020.
High School ni album ya pilli katika maisha ya muziki wa harmonize iliyobeba jumla ya mikwaju 20, ikitanguliwa na Afro East iliyotoka mwaka mmoja uliopita.