Msanii wa Bongofleva Ibraah amekana kupata mtoto na mwanamke anayefahamika kwa jina la Kim Mishepu ambaye alitoa taarifa za kuzaa nae mitandaoni mwishoni mwa mwaka 2021.
Katika mahojiano yake hivi karibuni Ibraah amesema taarifa hizo sio za kizushi kwa kusema kwamba ni kweli alikuwa na mototo aliyezaa na mwanamke aitwaye Pendo lakini kwa bahati mbaya alifariki akiwa na miezi mitano.
Utakumbuka mwanadada Kim Mishepu aliyedai kuwa alizaa na Ibraah alimtuhumu msanii huyo kuwa amemtelekeza pamoja na motto wake baada ya kusainiwa na lebo ya konde gang inayomilikiwa na Harmonize.