You are currently viewing IRENE NTALE AKERWA NA TABIA YA VIJANA WADOGO KUMTAKA KIMAPENZI KWENYE MITANDAO YA KIJAMII

IRENE NTALE AKERWA NA TABIA YA VIJANA WADOGO KUMTAKA KIMAPENZI KWENYE MITANDAO YA KIJAMII

Staa wa muziki nchini Uganda Irene Ntale amekuwa akisema kwamba yupo tayari kwa ajili ya ndoa na iwapo hilo litatimia anataka kuolewa na mwanaume wa ndoto yake. Lakini inaonekana mrembo huyo anafuatwa na vijana wadogo.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Irene Ntale amesema hayuko tayari kuchumbiana na vijana wadogo ambapo ametoa onyo kwao kuacha tabia ya kumsumbua kwenye mitandao yake ya kijamii kama hawajafikisha umri wa miaka 30.

Ikumbukwe Irene ntale amekuwa akisumbuka kumpata mwanaume atakayemuoa tangu aachane na aliyekuwa mchumba wake Jonathan Kyeyo. Jambo hilo lilimlazimu kutangaza kwamba yupo singo  na hilo limepelekea wanaume wa kila aina kuanza kumchumbia.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke