You are currently viewing IYANII ANYOSHA MAELEZO KUHUSU ISHU YA KUWA NUSU UCHI KWENYE UZINDUZI WA ALBUM YA ARROW BOY

IYANII ANYOSHA MAELEZO KUHUSU ISHU YA KUWA NUSU UCHI KWENYE UZINDUZI WA ALBUM YA ARROW BOY

Msanii wa lebo ya Utembe World, Iyanii ametetea hatua yake ya kuwa nusu uchi kwenye hafla ya uzinduzi wa album mpya ya bosi wake Arrow Boy.

Katika mahojiano yake ya hivi karibuni Iyanii amesema aliahamua kufanya hivyo kama njia ya kuonyesha ubunifu kwenye masuala ya mitindo na fasheini kwani ni kitu ambacho amekuwa akifanya tangu utotoni.

Hitmaker huyo wa ngoma ya “Pombe” amekanusha kutumia suala hilo kutengeneza mazingira ya kuzungumziwa kwenye vyombo vya habari nchini ikizingatiwa kwamba yeye ni moja kati ya wasanii wasiopenda kutumia kiki kutangaza muziki wake.

Utakukumbuka Iyanii ni moja kati ya wasaniii waliotumbuza  kwenye hafla ya uzinduzi wa album ya Focus ya Arrow boy Usiku wa kuamkia Machi 13 Jijini Nairobi.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke