Timu ya Taifa ya Japan imefanikiwa kutinga hatua ya 16 Bora ya michuano ya kombe la Dunia baada ya kuitandika Uhispania 2-1 katika mchezo wa mwisho wa kundi E
Ushindi huo umeifanya Japan kumaliza wakiwa vinara kwenye kundi hilo lililokuwa na vigogo vya Uhispania na Ujerumani waliopewa nafasi kubwa zaidi.
Ujerumani licha ya kuibuka na ushindi wa 4-2 dhidi ya Costa Rica wamefungashiwa virago kwenye michuano hiyo kwa kumaliza wa tatu kwenye kundi E