You are currently viewing JOVIAL AKANUSHA KUTOKA KIMAPENZI NA DJ SAMI FLINCH

JOVIAL AKANUSHA KUTOKA KIMAPENZI NA DJ SAMI FLINCH

Female singer kutoka Kenya Jovial amekanusha madai yanayotembea mtandaoni kuwa anatoka kimapenzi na DJ maarufu nchini Sami Flinch.

Katika kikao cha maswali na mashabiki zake kwenye mtandao wa Instagram Jovial amesema madai hayo hayana msingi wowote huku akisema ukaribu wao ulitokana na shughuli za kikazi ambazo walikuwa nayo kipindi cha nyuma.

Hitmaker huyo wa ngoma ya “Pita Nawe” amesema kwa ngazi aliyofika kwa sasa anahitaji zaidi pesa kuliko mpenzi huku akithibitisha kuwa hayupo kwenye mahusiano.

Hata hivyo amesema skendo za mtandaoni hazina nafasi kwa sasa katika maisha yake kwani anahitaji kuacha mashabiki wake wapate wanachostahili kupitia muziki wake.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke