You are currently viewing JULIANI AKIRI KUYUMBA KIUCHUMI

JULIANI AKIRI KUYUMBA KIUCHUMI

Mwimbaji Julius Owino almaarufu Juliani amekiri hadharani kuyumba kiuchumi baada ya walimwengu kumkejeli mtandaoni.

Katika video aliyochapisha kwenye instastory yake, Juliani amesema kuwa tatizo linalomkabili limechangiwa na hatua ya kutumia fedha zake kufadhili mipango yake bila wafadhili huku akifichua kuwa alichukua mikopo kwa ajili ya kukamilisha baadhi ya miradi.

Aidha amesema changamoto za kifedha anazokumbana nazo kwa sasa zimemfanya akose muda wa kukaa na mtoto wake huku akimshukuru mke wake Lilian Nganga kwa kumuelewa.

Katika hatua nyingine mwimbaji huyo amesema kuwa amejipa miaka 10 kutimiza ndoto aliyonayo kwa jamii yake ikiwemo kutengeneza ajira 10,000 na kutoa mikopo kwa wasanii.

Juliani, hata hivyo amebainisha kuwa licha ya kuyumba kiuchumi, bado ana uwezo wa kukidhi mahitaji yake ya msingi ambapo amewataka walimwengu kukoma kumfanyia mzaha mtandaoni kuhusiana na hali yake ya kiuchumi kwani inamuathiri kisaikolojia.

Elim Robert

Robert Elim is an Editor with high interest and knowledge in the entertainment space, an industry he has been actively part of since childhood. Leads to breaking stories are welcome at elimrobert@gmail.com & contact@urbanspice.co.ke